Tunafanya Nini
Utafiti na Ubunifu
Uendelezaji wa teknolojia na ubunifu unafanywa chini ya mada mbalimbali: Uboreshaji wa mazao, Agronomia, Ulinzi wa mazao, Usimamizi baada ya mavuno, Uchumi wa kijamii, Jinsia na Masoko, Usimamizi wa rasilimali za asili, Utoaji wa mashine za kilimo, na Uhandisi wa kilimo.
Uhifadhi wa Mbegu
Kuzalisha mbegu za kizazi cha awali (pre-basic na basic seed) na mbegu zilizothibitishwa (certified seed) za aina za mazao yaliyoboreshwa kwa wadau wengine katika mnyororo wa thamani ya mbegu. Aidha, TARI inahifadhi mbegu za aina mbalimbali za mazao ili kuhakikisha ubora na usafi wake.
Cheti cha Idhini ya Maadili
Hutoa idhini na kusimamia masuala ya maadili kwa taasisi za kimataifa na za ndani pamoja na watu binafsi wanaofanya utafiti wa kilimo katika Tanzania Bara.
Usajili wa Utafiti wa Kilimo
Usajili wa taasisi na watu binafsi wanaofanya shughuli au miradi ya utafiti wa kilimo katika Tanzania Bara.
Mafunzo
TARI hufanya mafunzo mbalimbali kwa wadau tofauti wa kilimo ili kuboresha usalama wa chakula, lishe, na kipato, pamoja na kupunguza kazi ngumu. Mafunzo haya kwa kawaida ni juu ya:
-
Mbinu Bora za Kilimo
-
Usimamizi baada ya mavuno
-
Kuongeza thamani
-
Uchumi wa kijamii
-
Kuingiza masuala ya jinsia
Huduma za Maabara
Kufanya uchambuzi wa sampuli za udongo na mimea ili kubaini virutubisho, utambuzi na uchunguzi wa wadudu na magonjwa, na DNA fingerprinting.
Ushauri
Huduma za kiufundi na ushauri kwa watu binafsi na taasisi.
Takwimu
Ukusanyaji, upangaji, na uchambuzi wa data za utafiti wa kilimo.